Showing posts with label TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label TANZANIA. Show all posts
Friday, 6 May 2016
HABARI: TANZANIA.
BALOZI mteule, Dk Asha-Rose Migiro ameapishwa na Rais John Magufuli kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na ameahidi utumishi uliotukuka utakaoendelea kuziunganisha nchi hizo mbili.
Taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, Ikulu, Gerson Msigwa mjini Dodoma jana ilieleza kuwa hafla ya kuapishwa kwa Dk Migiro ilifanyika jana katika Ikulu ndogo ya Chamwino, Dodoma na ilihudhuriwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.
Dk Migiro aliteuliwa na Rais kuchukua nafasi ya Balozi Peter Kallaghe aliyerudishwa nyumbani. Akizungumza baada ya kuapishwa, Dk Migiro alisema atahakikisha uhusiano na ushirikiano mzuri na wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na Uingereza unaimarishwa zaidi. Alitaja eneo mahususi la ushirikiano kuwa ni katika kuvutia uwekezaji, biashara na utalii baina ya nchi hizo mbili.
Saturday, 15 August 2015
MABADILIKO YA RATIBA MWENGE CATHOLIC UNIVERSITY.
MWECAU OPEN TIME TABLE FOR ACADEMIC YEAR 2015-2016
- Details
- Category: News and Events
- Published: 12 August 2015
To: All Students
From: DVCAA
Date: 12th August, 2015
Subject: MWECAU OPEN TIME TABLE
Your Kindly informed that due to the directives from the TCU, The opening date for the Students has changed and shall be as follows;-
- Non degree courses, (Certificates, Diplomas, Post Graduate, Masters and PhD) shall start the registration and Orientation for new academic year on Tuesday 15thSeptember 2015 to Saturday 19th September 2015 and lectures shall Begin onMonday 21st September 2015
- All Undergraduate students including new first year students shall start registration on Wednesday 28th October 2015 to Friday 30th October 2015 and lectures shall begin on 2nd November 2015
NB: The Supplementary Examinations shall be held on Monday 14th September 2015, and Graduation day shall be 31st October 2015
Monday, 10 August 2015
Thursday, 6 August 2015
CUF BADO IPO UKAWA.
CUF IMESEMA INAENDELEA KUBAKI UKAWA LICHA YA LIPUMBA KUJIUZULU
Baada ya Prof Ibrahimu Lipumba kujivua Uenyekiti wa CUF, Chama cha CUF kimesema kuwa kitaendelea kubaki UKAWA na kuulinda umoja huo. Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kaimu Mkurugenzi wa habari, uenezi na mawasiliano kwa umma Ismail Jussa inasema hivi
"Leo tarehe 6 Agosti, 2015 Profesa Ibrahim Lipumba aliitisha mkutano na waandishi wa habari katika Hoteli ya Peacock, mjini Dar es Salaam na kutangaza kwamba amejizulu nafasi yake kama Mwenyekiti wa Taifa wa Chama Cha Wananchi (CUF).
Sisi kama Chama tumezipokea taarifa hizo na tunayaheshimu maamuzi yake. Ni haki yake ya kikatiba na haki ya kidemokrasia kufanya maamuzi anayoyaona yana maslahi kwake.
Bila shaka, Profesa Ibrahim Lipumba amekifanyia kazi kubwa Chama chetu katika miaka 16 ambayo alikuwa Mwenyekiti wetu, nafasi iliyomfanya awe kiongozi wetu mkuu. Kwa nafasi yake hiyo, pia ametoa mchango mkubwa katika ujenzi wa demokrasia katika nchi yetu. Tunaithamini kazi hiyo na tutaendelea kumheshimu kwa utumishi wake mkubwa kwa Chama chetu na nchi yetu. Tunamtakia kila la kheri katika mipango yake ya baadaye.
Chama Cha Wananchi (CUF) ni taasisi na kinaendeshwa kitaasisi. Ndiyo maana maamuzi yake yote yamekuwa yakifanywa kitaasisi kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Chama. Kwa msingi huo, pamoja na ukweli kwamba kuondoka kwa Profesa Lipumba katika safu ya uongozi kutaacha pengo hasa katika kipindi hichi ambacho tunaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu, tunawahakikishia wanachama na wapenzi wa CUF na wananchi wa Tanzania kwa ujumla kwamba Chama hichi hakitayumba.
HONGERA Diamond.


Staa wa Bongo Fleva ambaye jina lake limebeba uzito mkubwa Afrika, Diamond Platnumz anayo furaha kushare na sisi hii good news… Post yake Instagram inasomeka hivi >>> ‘My mom’s face it’s enough to Express how i feell



SIASA TANZANIA.
Kumekuwa na stori nyingi ambazo zimeandikwa sana Magazetini kuhusu Umoja wa Vyama vya UKAWA, baada ya Mbunge wa Monduli kukaribishwa CHADEMA na UKAWA stori nyingine zikaanza kuchukua headlines kuhusu baadhi ya Viongozi waliopo Vyama vya UKAWA.
August 06 2015 nimeipata taarifa rasmi kutoka kwenye Kikao ambacho Prof. Lipumbaamekifanya Dar, ametangaza rasmi kujiuzulu nafasi yake ya Uenyekiti wa Chama hicho.
Wednesday, 5 August 2015
CCM, TANZANIA.
MWENYEKITI wa Taifa wa CCM, Rais Jakaya Kikwete amesema chama hicho sio chama cha mchezo na kuvionya vyama vya upinzani kuwa watakiona cha mtema kuni katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu.
Amesema CCM itapata ushindi katika uchaguzi huo kwa kuwa imejipanga kwa hoja na imeleta maendeleo nchini, huku akieleza kuwa wapo watu wenye tamaa ya uongozi ambayo imekithiri.
Aliungwa mkono na Mgombea Urais wa CCM, Dk John Magufuli aliyesema chama hicho kitashinda na haoni wa kuwashinda, huku akiahidi kuwa atakuwa mtumishi wa Watanzania kwani anazijua shida zao.
Rais Kikwete aliyasema hayo jana katika Ofisi Ndogo za CCM, Mtaa wa Lumumba, Dar es Salaam ambako alikuwapo kumpokea Dk Magufuli na Mgombea Mwenza Samia Suluhu Hassan baada ya kutoka kuchukua fomu katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katikati ya Jiji ili kuomba kuidhinishwa kuwa wagombea.
“Sasa kazi ndio imeanza rasmi. Dodoma zile zilikuwa rasharasha. CCM sio chama cha mchezo. Watakiona cha mtema kuni. Kama ni mpira wa miguu, basi tumefunga bao wakiwa wamesimama. Tumejiandaa vya kutosha na kushinda tutashinda. Uzoefu, maarifa na uwezo wa kushinda tunao,” alisema Rais Kikwete na kuongeza: “Nawataka wanaCCM kujipanga, msimdharau yeyote hata mpinzani akiwa mdogo shughulikeni naye. Tumejipanga kwa hoja, tunazo hoja za kuzungumza. Nchi tulivu na maendeleo yanaonekana na duniani kote wanajua kuwa Tanzania inafanya vizuri. Tunao utawala bora, demokrasia na uhuru wa habari. “Hata duniani wanajua hilo na wanaona fahari kushirikiana na Tanzania. Lakini wapo watakaokuwa na tamaa tu, duniani wapo watu wameumbwa hivyo, wengine wanayo tamaa hadi imekithiri, imevuka mipaka,” alieleza Rais Kikwete mbele ya maelfu ya viongozi, wanachama na mashabiki wa chama hicho tawala.
Rais Kikwete aliyefuatana na mkewe Mama Salma, alikatiza hotuba yake na kuliomba kundi la Tanzania One Theatre (TOT) kuimba wimbo wa “Waache waseme CCM ina wenyewe,” ambao alishiriki kucheza na mwisho wa wimbo huo, alisema: “Ni ushindi wa uhakika, hauna hatihati. CCM shangilia ushindi unakuja.”
Kabla ya kumkaribisha Dk Magufuli na Samia, Mwenyekiti huyo wa CCM alisema uzinduzi wa kampeni za urais kwa chama hicho utafanyika Agosti 22, mwaka huu na watatangaza wapi uzinduzi huo utafanyika kwani Viwanja vya Jangwani kwa sasa havina fursa hiyo kwa kujengwa miradi ya mabasi ya haraka na wafanyabiashara wadogo.
Alishuka jukwaani saa saba kamili mchana baada ya kuwatambulisha wagombea hao wawili, ambapo Samia kwa upande wake alisema haoni sababu ya CCM kushindwa kutokana na jinsi kazi ya jana ya kwenda kuchukua fomu ilivyokusanya maelfu ya wanachama, wapenzi na mashabiki wa chama hicho tawala.
Lakini, Dk Magufuli ambaye aliwasili Lumumba saa 4.47 asubuhi ili kwenda kuchukua fomu hizo, alisisitiza kauli ya Rais Kikwete kuwa CCM itashinda kwani chini ya uongozi wa rais huyo anayemaliza muda wake kikatiba, mambo mengi mazuri yamefanywa ambayo yanawafanya watembee kifua mbele.
“Kujitokeza kwenu kwa wingi leo ni ushahidi mwingine kuwa CCM itaendelea kutawala. Niwathibitishie kuwa shida za Watanzania nazijua, mategemeo ya Watanzania ninayo, na ipo misingi mizuri imewekwa chini ya Rais Kikwete. “Nawaahidi nitakuwa mtumishi wenu sababu ninazijua shida za Watanzania. Watanzania wana tatizo la ajira, hawataki kero za ovyo kama kukimbizana na mama ntilie na bodaboda. Wanataka uchumi wao uwe mzuri, wanataka maisha mazuri zaidi. Nitayasimamia, nawahakikishia sababu kero hizo nazijua,” alisema Dk Magufuli.
“Nimekuwa mbunge kwa miaka ishirini na nimekuwa Waziri. Nimepata uzoefu kwa Rais Kikwete, Mzee Mwinyi, Mzee Mkapa, Mzee Nyerere, na viongozi wengine. Niko tayari kukipokea kijiti kwa mikono miwili. Nataka Mwenyekiti kukuhakikishia kuwa tutashinda, sioni wa kutushinda,” alisema Dk Magufuli huku akirudia maneno ya “sioni wa kutushinda” mara tatu.
Alisema atakuwa mtumishi wa Watanzania wote bila kujali dini, kabila, itikadi kwa sababu maendeleo ni ya wote, lakini akawataka wadumishe umoja na amani, na kuwaahidi kuwa hatawaangusha.
Awali, baada ya kuwasili Lumumba, alipokewa na Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana na kisha kuingia katika ofisi hizo na walitoka nje saa 5.19 asubuhi kuanza safari ya kwenda NEC, ambako mgombea huyo na mgombea mwenza walipanda gari la wazi aina ya Toyota Landcruiser lenye namba za usajili TY813 DEQ mali ya CCM.
Maelfu ya wanaCCM wakiongozwa na Kinana, Naibu Katibu Mkuu Bara, Rajab Luhavi, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Mwenyekiti wa Mkoa, Ramadhani Madabida walitembea kwa miguu wakiwa mbele ya gari la wagombea wakipita barabara za Morogoro, Bibi Titi Mohammed, Ohio hadi Garden Avenue zilipo ofisi za Tume.
Katika msafara huo walikuwapo viongozi wengine waandamizi wa CCM, mawaziri na wabunge; miongoni mwao January Makamba, Jerry Silaa, Abdallah Bulembo, Dk Asha-Rose Migiro, Sophia Simba, Amina Makilagi, Dk Fenella Mukaranga, Hawa Ghasia, Muhammed Seif Khatib, Zakia Meghji, Steven Wassira na Angella Kizigha.
Pia, Mussa Azzan Zungu, Abbas Mtemvu, Janeth Masaburi, Didas Masaburi, Pindi Chana, Monica Mbega, Mary Chatanda na Betty Machangu wakati Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara Phillip Mangula alibaki Lumumba pengine kumpokea Mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete.
Friday, 31 July 2015
BVR DAR
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeongeza siku nne zaidi kwa wakazi
wa Jiji la Dar es Salaam, kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la
Wapiga Kura kwa Mfumo wa Kielektroniki (BVR).
Kwa ratiba iliyotolewa awali na NEC, leo ndio ilikuwa siku ya mwisho kwa wakazi wa jiji hilo kubwa nchini, kujiandikisha kwenye daftari hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva alisema wameongeza siku hizo kutokana na mwitikio mkubwa wa wananchi ulioonekana katika vituo mbalimbali vya kujiandikisha.
Alisema uandikishaji huo kwa nchi nzima ulianza Februari 23, mwaka huu mkoani Njombe na mpaka Julai 29, takwimu zinaonesha jumla ya wananchi 18,826,718 wameandikishwa huku lengo likiwa ni kuandikisha wananchi milioni 23.
Aliongeza kuwa kutokana na changamoto mbalimbali zilizojitokeza, ikiwemo ya mashine, Tume iliweza kuongeza mashine ili kuharakisha kazi hiyo kwa Jiji la Dar es Salaam.
“Tulianza na mashine 250 tu, baada ya uandikishaji kwa mkoa wa Njombe tuliendelea kuongeza mashine na mpaka sasa tuna mashine 8,000 ambazo tuna uhakika zitafanikiwa kukamilisha uandikishaji kwa siku zilizobakia,” alisema Lubuva.
Pia, alisema ili kuhakikisha kila mtu anajiandikisha vizuri na kuandika kumbukumbu sahihi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi itaonesha majina ya wananchi waliojiandikisha na taarifa zao ili kila mtu aangalie kama kumbukumbu zake zipo sahihi.
“Tumeamua kuonesha daftari hili na tutaanza Agosti Mosi katika mikoa ambayo tayari wamekamilisha uandikishaji na endapo kutakuwa na tatizo lolote lifanyiwe marekebisho na kila mtu atambue alipojiandikisha ili aweze kupata nafasi ya kupiga kura,” Lubuva alisema.
Aidha, alisema suala la kujiandikisha kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, si la NEC, bali ni la Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambayo inapaswa kupanga utaratibu na ratiba kuwawezesha wanafunzi hao, kujiandikisha katika eneo ambalo atakuwepo ifikapo Oktoba 25.
“Suala la wanafunzi kujiandikisha naona sasa hivi linachukuliwa kisiasa. Kila mwanafunzi anapaswa kujiandikisha mahali atakapokuwa Oktoba 25 na si jukumu letu kujua ni wapi mwanafunzi atakuwepo, kila mmoja ni mtu mzima na anapaswa kujiandikisha,” alisema Lubuva.
Pia, alisema kuhusu sula la wahamiaji kujiandikisha, kila mwananchi anapaswa kumtambua mwenzake ili kuepuka kumuandikisha mtu ambaye si Mtanzania.
“Mkituachia Tume peke yetu, kwakweli hatutaweza na ndio maana katika vituo kuna mawakala ambao wanapaswa kutambua yupi ni mkazi na yupi anazamia,” alisema Mwenyekiti huyo wa NEC.
Wakizungumzia hatua hiyo ya NEC ya kuongeza siku nne zaidi za kujiandikisha, wananchi wengi waliozungumza na gazeti hili, walilalamikia hatua hiyo wakisema siku nne zilizoongezwa ni chache na ni vigumu watu wote kupata nafasi.
Hamidu Baruani, mkazi wa Majohe wilayani Ilala, aliliambia gazeti hili kuwa siku zilizoongezwa bado ni chache, ukizingatia kuwa watu wengi bado hawajaandikishwa.
Aliongeza kuwa kumekuwepo na uhaba wa mashine na waandikishaji wamekuwa wanaandikisha watu kwa taratibu, hatua inayolazimu baadhi ya watu kulala vituoni, wakisubiri kuandikishwa bila mafanikio.
“Siku ni chache, kwa kweli kama mimi nilikaa sana kwenye kituo na nyumbani kwangu nilitoka saa nane usiku, kitendo ambacho pamoja na changamoto nyingine pia kilihatarisha maisha yangu,” alisema Baruani.
Aidha, Moses John mkazi wa Yombo wilayani Ilala, alisema kumekuwa na vurugu katika maeneo ya kujiandikisha, kitendo kinachosababisha watu wengi kushindwa kujiandikisha. “Mimi sijafanikiwa kujiandikisha, kila nikifika fujo tu watu ni wengi, ila naamini katika siku hizi zilizoongezwa, nitafanikiwa kujiandikisha japo siku hizo bado ni chache,” alisema John.
Kwa upande mwingine, NEC imewashukuru wananchi wa Dar es Salaam kwa kuwa wavumilivu wakati wa uandikishaji na wametakiwa kuendelea kutoa ushirikiano ili kufanikisha uandikishaji huo.
Kwa ratiba iliyotolewa awali na NEC, leo ndio ilikuwa siku ya mwisho kwa wakazi wa jiji hilo kubwa nchini, kujiandikisha kwenye daftari hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva alisema wameongeza siku hizo kutokana na mwitikio mkubwa wa wananchi ulioonekana katika vituo mbalimbali vya kujiandikisha.
Alisema uandikishaji huo kwa nchi nzima ulianza Februari 23, mwaka huu mkoani Njombe na mpaka Julai 29, takwimu zinaonesha jumla ya wananchi 18,826,718 wameandikishwa huku lengo likiwa ni kuandikisha wananchi milioni 23.
Aliongeza kuwa kutokana na changamoto mbalimbali zilizojitokeza, ikiwemo ya mashine, Tume iliweza kuongeza mashine ili kuharakisha kazi hiyo kwa Jiji la Dar es Salaam.
“Tulianza na mashine 250 tu, baada ya uandikishaji kwa mkoa wa Njombe tuliendelea kuongeza mashine na mpaka sasa tuna mashine 8,000 ambazo tuna uhakika zitafanikiwa kukamilisha uandikishaji kwa siku zilizobakia,” alisema Lubuva.
Pia, alisema ili kuhakikisha kila mtu anajiandikisha vizuri na kuandika kumbukumbu sahihi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi itaonesha majina ya wananchi waliojiandikisha na taarifa zao ili kila mtu aangalie kama kumbukumbu zake zipo sahihi.
“Tumeamua kuonesha daftari hili na tutaanza Agosti Mosi katika mikoa ambayo tayari wamekamilisha uandikishaji na endapo kutakuwa na tatizo lolote lifanyiwe marekebisho na kila mtu atambue alipojiandikisha ili aweze kupata nafasi ya kupiga kura,” Lubuva alisema.
Aidha, alisema suala la kujiandikisha kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, si la NEC, bali ni la Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambayo inapaswa kupanga utaratibu na ratiba kuwawezesha wanafunzi hao, kujiandikisha katika eneo ambalo atakuwepo ifikapo Oktoba 25.
“Suala la wanafunzi kujiandikisha naona sasa hivi linachukuliwa kisiasa. Kila mwanafunzi anapaswa kujiandikisha mahali atakapokuwa Oktoba 25 na si jukumu letu kujua ni wapi mwanafunzi atakuwepo, kila mmoja ni mtu mzima na anapaswa kujiandikisha,” alisema Lubuva.
Pia, alisema kuhusu sula la wahamiaji kujiandikisha, kila mwananchi anapaswa kumtambua mwenzake ili kuepuka kumuandikisha mtu ambaye si Mtanzania.
“Mkituachia Tume peke yetu, kwakweli hatutaweza na ndio maana katika vituo kuna mawakala ambao wanapaswa kutambua yupi ni mkazi na yupi anazamia,” alisema Mwenyekiti huyo wa NEC.
Wakizungumzia hatua hiyo ya NEC ya kuongeza siku nne zaidi za kujiandikisha, wananchi wengi waliozungumza na gazeti hili, walilalamikia hatua hiyo wakisema siku nne zilizoongezwa ni chache na ni vigumu watu wote kupata nafasi.
Hamidu Baruani, mkazi wa Majohe wilayani Ilala, aliliambia gazeti hili kuwa siku zilizoongezwa bado ni chache, ukizingatia kuwa watu wengi bado hawajaandikishwa.
Aliongeza kuwa kumekuwepo na uhaba wa mashine na waandikishaji wamekuwa wanaandikisha watu kwa taratibu, hatua inayolazimu baadhi ya watu kulala vituoni, wakisubiri kuandikishwa bila mafanikio.
“Siku ni chache, kwa kweli kama mimi nilikaa sana kwenye kituo na nyumbani kwangu nilitoka saa nane usiku, kitendo ambacho pamoja na changamoto nyingine pia kilihatarisha maisha yangu,” alisema Baruani.
Aidha, Moses John mkazi wa Yombo wilayani Ilala, alisema kumekuwa na vurugu katika maeneo ya kujiandikisha, kitendo kinachosababisha watu wengi kushindwa kujiandikisha. “Mimi sijafanikiwa kujiandikisha, kila nikifika fujo tu watu ni wengi, ila naamini katika siku hizi zilizoongezwa, nitafanikiwa kujiandikisha japo siku hizo bado ni chache,” alisema John.
Kwa upande mwingine, NEC imewashukuru wananchi wa Dar es Salaam kwa kuwa wavumilivu wakati wa uandikishaji na wametakiwa kuendelea kutoa ushirikiano ili kufanikisha uandikishaji huo.
Thursday, 30 July 2015
SIASA TANZANIA

Hatua ya Lowassa kuchukua fomu ya urais inakuja siku moja baada ya yeye na mke wake Regina Lowassa, kujiunga na chama hicho katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam ambamo aliahidi kuiongezea Chadema nguvu ya wanachama kuelekea ushindi katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu kuiondoa CCM madarakani.
Taarifa ya Lowassa kuchukua fomu hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Makao Makuu ya Chama hicho Kinondoni jijini Dar es Salaam.
“Kesho saa 5 asubuhi hapa makao makuu ya chama, Mheshimiwa Edward Ngoyai Lowassa atachukua fomu ya kugombea urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chadema. Kutakuwa na shamrashara nyingi sana. Na kutakuwa na matokeo mengi baada ya kesho,” amesema Mwalimu.
Aidha, Mwalimu ametoa ufafanuzi kuhusu uwepo wa minong’ono kwamba Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika na Tundu Lissu, Mwanasheria wa chama hicho kwamba walisusia tukio la Lowassa kujiunga na Chadema.
“Jana ilipita minong’ono mingi tu, katibu mkuu wetu yupo kwenye majukumu mengi. Katika kipindi hiki cha uchaguzi tuna mambo mengi. Hatuwezi wote kuwa pamoja. Tunagawanyika kulingana na programu tulizonazo,” amefafanua Mwalimu.
Monday, 27 July 2015
CHADEMA.
Jiwe walilokataa waashi,,limekuwa jiwe kuu la pembeni.Ninakutakia afya njema na mafanikio kamanda Edward Ngoyai Lowassa,,,,,Hakika wewe ndiwe tunayekusubiria.Imani ya watanzania ipo kwako,,Edward Edward Ngoyai Lowassa,,,tunakuamini.
Wednesday, 22 July 2015
JAMES LEMBELI ATANGAZA RASMI KUJIUNGA CHADEMA
Aliyekuwa Mbunge wa KahamaJamse Lembeli (CCM) ameongea na waandishi
wa habari na kutanga kuhama chama cha CCM na kujiunga na CHADEMA na huku
akitangaza nia kugombea Jimbo la kahama mjini huku akiwataka wanakahama
wamuunge mkono kugombea jimbo hilo.
Akielezea nia yake ya kujiunga na CHADEMA ni kuona chama hiko kina mienendo mizuri na hakijihusishi na rushwa kama ilivyokuwa katika chama cha CCM. Huku akieleza kuwa katika Bunge la katiba yeye ndio alikua mbunge wa kwanza wa CCM kupiga kura ya wazi huku akiunga mkono katiba pendekezo ya Jaji Warioba.
Akielezea nia yake ya kujiunga na CHADEMA ni kuona chama hiko kina mienendo mizuri na hakijihusishi na rushwa kama ilivyokuwa katika chama cha CCM. Huku akieleza kuwa katika Bunge la katiba yeye ndio alikua mbunge wa kwanza wa CCM kupiga kura ya wazi huku akiunga mkono katiba pendekezo ya Jaji Warioba.
Thursday, 16 July 2015
SIASA, TANZANIA.
Dodoma. CCM stalwart Pancras Ndejembi has challenged Monduli MP and former Prime Minister Edward Lowassa to publicly declare his support for the ruling party’s presidential candidate, Dr John Magufuli.
Speaking at his Uzunguni home yesterday, Mr Ndejembi, said he was among those who were supporting Mr Lowassa and he believed that the former premier was capable of leading the country successfully.
However, since his party has already decided otherwise he has already forgotten about his support for Lowassa and he has thrown his weight behind the candidate nominated by the party.
He gave the statement amid speculations and rumours that Mr Lowassa was thinking of decamping to the Opposition to show his discontent over the way CCM treated him because he believes that he was an aspirant with biggest support.
“It is not a secret that I supported Lowassa; I was exercising my democratic right. But I cannot leave CCM simply because the aspirant I was supporting has not been nominated. I will stay in CCM and Magufuli is my candidate,” he said adding:
“Our party has its regulations and system which must be respected. All members are supposed to trust and respect decisions made by the party. I would like to appeal to Mr Lowassa not to decamp, he will lose his respect and trust.” He said, as a CCM Trustees he was not barred to support one aspirants and that is why he earlier supported Mr Lowassa.
Tuesday, 14 July 2015
SIASA, UKAWA TANZANIA.

Uongo ukiachwa ukasemwa sana bila kusahihishwa unaweza kugeuka kuwa ukweli.
Tungependa kusahihisha propaganda nyepesi zinazoendelea kuenezwa ili kuusaidia umma usiendelee kupotoshwa kwa mambo yasiyokuwa ya msingi huku kukiwa na mambo makubwa yanayohitaji 'attention' ya Watanzania kuamua mustakabali sahihi wa nchi yao kwa kuchagua MABADILIKO kupitia uchaguzi wa kihistoria hapo Oktoba 25.
1. Zipo taarifa zinaendelea kuenezwa kuhusu makada wa CCM wakiongozwa na Edward Lowassa kuwa wana mpango wa kuhamia CHADEMA. Hadi sasa tunaziona habari hizo kupitia mitandaoni na kwenye vyenye mainstream media. Bila shaka wenye taarifa sahihi za mipango hiyo ni hao hao wanaozieneza. Nasi hatuwajibiki kabisa kuwasaidia kutoa uhakika wa uenezi huo wanaofanya kwa maslahi wanayoyajua.
2. Viongozi wakuu wa chama wakiongozwa na Mwenyekiti wa Taifa Freeman Mbowe na Katibu Mkuu Dk. Willibroad Slaa wamekuwa wakiendelea na majukumu yao mbalimbali kwa kadri ya nafasi zao na ratiba za chama hususan wakati kama huu kuelekea defining moments za uchaguzi mkuu ambapo mara kadhaa wamekuwa katika vikao na viongozi wakuu wenzao katika UKAWA ili kutafuta mwelekeo sahihi kwenda Oktoba 25.
Wanaoeneza habari kwamba Mkiti Mbowe na KM Dk. Slaa wamekuwa na mtafaruku eti kwa sababu ya 'ujio dhanifu' wa Lowassa basi watu hao watakuwa hawajui utaratibu wa utendaji kazi wa Chama kwa ujumla na hususan Viongozi hao wawili ambao siku zote hufanya kazi kwa maelewano ya hali ya juu sana kiasi cha kuendelea kuwa sehemu ya uimara wa CHADEMA.
3. Propaganda hizo zinazojengwa katika misingi ya siasa nyepesi zimekwenda mbali hadi kumsemea uongo mmoja wa waasisi wa CHADEMA Mzee Mtei eti amekodiwa ndege kuja kutuliza mtafaruku.
3. Tunajua lengo la upotoshwaji huo ni kutaka kuwachaganya Watanzania wanaojiandaa kuiondoa CCM madarakani mwaka huu. Waenezaji uongo wanataka kuwaaminisha Watanzania wanaowaka moto wa mabadiliko kuwa CHADEMA nayo imegawanyika kama ilivyo kwa CCM ambayo imesambaratika juzi Dodoma kiasi cha wajumbe kumzomea Mwenyekiti wao wa chama.
4. CHADEMA iko imara kuliko wakati mwingine wowote ule, hasa katika kipindi hiki ambapo inaendelea kujiandaa kuwatumikia Watanzania na kupanga mikakati mbalimbali, kwa kushirikiana na washirika wenza kwenye UKAWA, kuikabili CCM iliyomeguka vipande vipande na kuiondoa madarakani.
NB; Kuhusu #UKAWA Julai 14
Kama ambavyo Mwenyekiti Mwenza wa UKAWA Prof. Ibrahim Haruna Lipumba alisema Jumamosi usiku alipozungumza na waandishi wa habari kuwa leo umoja huo utafikia na kutangaza kwa umma makubaliano juu ya mambo makubwa mawili;
1. Mgombea mmoja wa urais
2. Majimbo yaliyokuwa yamesalia katika mgawanyo kwa maana ya kusimamisha Mgombea mmoja
Aidha, Prof. Lipumba alisema kuwa UKAWA wameshafanikiwa kufikia mwafaka katika majimbo kwa asilimia 97 na sehemu iliyobakia ni ile ambayo itahitaji mashauriano au (bilateral) mwafaka kati ya vyama viwili katika majimbo fulani fulani ambapo vyama hivyo vilikuwa bado vinapitia vigezo vilivyokubalika.
Tangu asubuhi ya leo vikao vimekuwa vikiendelea. Majadiliano yamekwenda vizuri kabisa. Baadae Summit (kikao cha Viongozi wakuu) itakutana kwa ajili ya wayfoward na kuzungumza makubaliano kwa Vyombo vya Habari kwa ajili ya Watanzania.
Vyombo vya Habari vitataarifiwa muda na mahali ambapo Summit ya UKAWA itakutana nao kwa ajili ya taarifa hiyo inayosubiriwa na umma wa Watanzania.
UKAWA, TANZANIA.
UPATIKANAJI wa mgombea mmoja wa urais kupitia vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), umeendelea kujadiliwa katika kikao cha siri cha vyama hivyo, huku hali ikijionesha kuwepo kwa mvutano baina ya vyama vikuu katika umoja huo.
Jana baadhi ya vyombo vya habari vilidai kuwa umoja huo, unaoundwa na Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD, ulishaafiki Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa, ndio apeperushe bendera ya vyama hivyo na kwamba uamuzi huo ungetangazwa jana.
Lakini umoja huo ulikutana kwa ajili ya kujadiliana na kutoa tamko juu ya makubaliano yao ya ugawanaji wa majimbo na mgombea rais atakayesimamishwa tangu saa nane mchana mpaka saa mbili usiku bila kutoa tamko lolote.
Mkutano huo uliofanyika katika jengo jipya la Kisenga LAPF liliopo Kijitonyama ambako waandishi walipiga kambi, lionekana kukumbwa na sintofahamu kwa wanahabari ambao walikaa zaidi saa tano kusubiri kile kitakachoamuliwa na umoja huo.
Hata hivyo baadhi ya wajumbe wa mkutano huo akiwemo Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema) na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) walitoka mapema kabla ya kikao hicho kumalizika hali iliyozua maswali zaidi.
Alipohojiwa na waandishi wa habari kuhusu kutoka katika mkutano huo na kuacha ukiendelea, Kafulila alisema bado hawajafikia uamuzi ila watakachoafikiana kitatangazwa na viongozi wa umoja huo na si yeye kwa kuwa hana mamlaka ya kusemea viongozi wa umoja huo.
Viongozi wa umoja huo waliohudhuria mkutano huo ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Katibu Mkuu wake, Dk Willbrod Slaa, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa NLD, Dk Emmauel Makaidi na Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Mosena Nyambabe.
Monday, 13 July 2015
SIASA TANZANIA.
DAKTARI wa Kemia, John Pombe Joseph Magufuli (56) ndiye mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu mwaka huu.
Waziri huyo wa Ujenzi aliwashinda wagombea wenzake wawili, Balozi Amina Salum Ali na Dk Asha-Rose Migiro kupata uteuzi huo wa CCM.
Alishinda katika Mkutano Mkuu Maalumu uliofanyika juzi na jana kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Dodoma (DCC) eneo la Makulu katika Makao Makuu ya Tanzania, Dodoma.
Mbunge huyo wa Chato katika Mkoa wa Geita, alipata kura 2,104 kati ya kura halali 2,416 zilizopigwa na wajumbe 2,422 wa mkutano huo. Ushindi wake kwa mujibu wa Spika wa Bunge, Anne Makinda ni asilimia 87.1, huku wenzake, Balozi Amina akipata kura 253 (asilimia 10.5) na Dk Migiro kura 59 (asilimia 2.4).
Hii ni mara ya kwanza kwa wanawake kufika hatua ya tatu bora katika mchakato wa kumpata mgombea wa urais ndani ya CCM. Makinda aliyekuwa miongoni mwa jopo la kuhesabu kura hizo, alisema kura sita ziliharibika wakati alipotangaza matokeo jana saa 6.50 mchana.
Wakati akitangaza matokeo hayo, Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Rais Kikwete alimtaka kusoma polepole matokeo hayo kwa wajumbe waliokuwa wakimsikiliza kwa makini. Wagombea hao watatu walipigiwa kura juzi usiku baada ya kuteuliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa kwa kupigiwa kura miongoni mwa wagombea watano waliopitishwa na Kamati Kuu ya CCM.
Dk Magufuli aliongoza akifuatiwa na Balozi Amina, Dk Migiro, na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ambao kura hazikutosha.
Dalili njema kwa Dk Magufuli kushinda uteuzi huo, zilionekana tangu juzi usiku wakati akiingia katika ukumbi wa mkutano, alishangiliwa mno na wajumbe hao na kuzunguka kila kona kuwasalimu.
Alilazimishwa na Katibu wa NEC wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye kurudi katika eneo lake kwenye mkoa wake wa Geita kukaa, ili kuruhusu mkutano huo uendelee kwa utulivu. Jana, baada ya kutangazwa mshindi, aliitwa mbele ya meza kuu na Rais Kikwete, na alipanda eneo hilo saa 12.58 mchana na dakika mbili baadaye alifika kwa Rais Kikwete, wakakumbatiana na kisha akainuliwa mkono kutambulishwa kwa wajumbe.
Ilipotimu saa 7.05, bendi ya Tanzania One Theatre (TOT), ikimkosa kiongozi wake mahiri, Kapteni John Komba aliyefariki dunia mapema mwaka huu, iliongoza kuimba wimbo maarufu wa “Sasa Kumekucha, Jogoo ameshawika Dodoma.”
Baadaye, mkewe Dk Magufuli, Janeth alipanda katika meza kuu na muda mfupi baadaye, mke wa Rais, Mama Salma Kikwete aliungana naye hapo, na sherehe zikaendelea hadi Kamati Kuu ilipokwenda kushauriana kuhusu jina la Mgombea Mwenza.
Kwa ushindi wake, Dk Magufuli anasubiri baraka za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kuidhinisha jina lake ili apeperushe bendera ya CCM katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu. Atapambana na vyama vya upinzani vinavyojiandaa kusimamisha mgombea mmoja chini ya mwavuli wa kinachoitwa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Aidha, Dk Magufuli mwenye Shahada ya Uzamivu ya Kemia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, anajiandaa kurithi mikoba ya Rais Kikwete endapo atashinda uchaguzi huo na kuongoza Serikali ya Awamu ya Tano.
Mbali ya kuwa Waziri wa Ujenzi kuanzia mwaka 2010 hadi sasa, Dk Magufuli aliyezaliwa Oktoba 29, 1959 wilayani Chato, amewahi kuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, zote katika Serikali ya Rais Kikwete.
Katika Awamu ya Tatu, alikuwa Waziri wa Ujenzi kuanzia mwaka 2000 hadi 2005 na Naibu Waziri wa wizara hiyo kuanzia 1995 hadi 2000. Alipopewa fursa ya kuzungumza na wajumbe wenzake wa Mkutano Mkuu Maalumu, Dk Magufuli alisema, “Nimehemewa sana.”
Alisema jana ilikuwa siku muhimu sana katika historia ya chama hicho na kwake mwenyewe. “Jana (juzi) nilisema nitumieni nami nitawatumikia, nawashukuru kwa kura za kishindo, sina cha kuwalipa isipokuwa nasema ‘asanteni sana, sana, sana.”
Aliahidi kuwatumikia wanaCCM na Watanzania kwa ujumla kwa nguvu zake zote, uwezo wake na vipaji vyote alivyopewa na Mwenyezi Mungu katika kuongoza baada ya kupewa heshima hiyo kubwa. Alisema CCM ni moja na wanaCCM ni wamoja, hivyo anatarajia kufasiri kauli hiyo kuwa ushindi wa kishindo katika Uchaguzi Mkuu ujao.
“Tudhihirishe kwa vitendo kuwa Umoja ni Ushindi. Wenzangu 38, viongozi, wanachama na mashabiki wa chama chetu tuungane pamoja ili ushindi wa chama chetu uwe mkubwa,” alifafanua.
Alisema uimara wa chama, uongozi imara na madhubuti na hamasa ya juu, pamoja na sera zake, ndio umeifanya CCM iwe na heshima ndani na nje ya nchi, na kwa kufuata taratibu za demokrasia ndani ya chama, inaonesha ni chama kilichokamaa. “Mtandao wetu wa ushindi ni mmoja. Nitafanya kila jitihada kuzitetea, kuzifafanua na kuzilinda sera hizi nzuri.
Asanteni kwa mchakato huu. “Niwathibitishie kwamba nitakuwa nanyi kweli kweli, nitakuwa mtumishi wenu,” alisema Dk Magufuli na kuongeza kuwa mchakato wa uteuzi wake ulikwenda vizuri na wagombea wenzake wote 38 wanaungana pamoja.
SIASA TANZANIA.
BARAZA la Ushauri la Chama Cha Mapinduzi (CCM), lenye wajumbe wazee wenye uzoefu, jana lilizima hoja kinzani ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), ambazo zilikuwa zinataka kurejeshwa kwa jina la Edward Lowassa katika kuwania uteuzi wa urais.
Waziri Mkuu wa zamani, Lowassa ni miongoni mwa wanachama 33 wa CCM waliochujwa na Kamati Kuu usiku wa kuamkia jana.
Lakini kukatwa kwa jina la Lowassa, kulizua maneno na sintofahamu miongoni mwa wajumbe wa NEC na walionesha fadhaa yao wakati wa ufunguzi wa kikao walipoimba wimbo wa “Tuna imani na Lowassa,” wakati wakuu wa CCM na viongozi wastaafu walipoingia kikaoni.
Lakini wakati wa kikao hicho ambacho waandishi wa habari hawakuruhusiwa kuingia, chanzo chetu kimeeleza kuwa wazee hao walituliza mambo wakisisitiza Katiba ya CCM na maslahi ya chama, ni muhimu kuliko maslahi binafsi au kingine chochote kile.
Wazee
Miongoni mwa waliozungumza ni marais wastaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa.
Wengine ni Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, Makamu Mwenyekiti mstaafu wa CCM John Malecela, na wabunge Christopher ole Sendeka na Livingstone Lusinde ‘Kibajaji.”
Wote katika hoja zao waliunga mkono uamuzi wa kumchuja Lowassa na kutetea maslahi mapana ya Chama na Katiba ya chama hicho kikongwe.
Malecela ambaye amerejea nchini juzi akitokea London kwa matibabu, alisikika akisema CCM ni muhimu zaidi kuliko mtu yeyote na kwamba kama kuna mtu anajiona ni muhimu zaidi, atoke.
Karume katika mchango wake, alieleza kuwa ni muhimu kuwa na mapenzi yasiyopitiliza kwa baadhi ya wanachama wenzao.
Mzee Mwinyi, Karume, Mkapa na Malecela, Pius Msekwa pamoja na Dk Salmin Amour Juma ambaye ni mgonjwa, wanaunda Baraza la Ushauri la Wazee wa CCM, lililoundwa miaka ya karibuni.
Wote hao isipokuwa Dk Salmin walihudhuria kikao cha Kamati Kuu juzi usiku pamoja na NEC jana na michango yao ndiyo iliyosaidia kwa kiasi kikubwa wajumbe kukubaliana na uteuzi wa CC.
Sendeka kwa upande wake, alieleza kuwa hali inayotokea sasa ni kutokana na kukiukwa kwa misingi ya chama hicho na kwamba kimeingiliwa na baadhi ya watu ambao wanataka kukivuruga.
Lusinde alisikika akisema kuwa mvutano uliotokea kwa wanachama hao ni kuwa baadhi yao wanatumiwa na wamehongwa fedha.
Kutokana na hali hiyo, NEC hatimaye ilikubaliana na uamuzi wa CCM wa kumchuja Lowassa, ambaye amechujwa pamoja na majina mengine makubwa yakiwamo ya Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Mtafaruku asubuhi
Awali, asubuhi baadhi ya wafuasi wa Lowassa walipaza sauti wakisema hawakubaliani na uteuzi wa CC na kudai kuwa watafanya mabadiliko makubwa ndani ya NEC, jambo lililoshindikana.Kwa uamuzi wa NEC, majina matano yaliyotoka CC yalipigiwa kura kuanzia saa 10.45 jioni.
Katibu wa NEC wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, aliwaambia waandishi wa habari saa 10.50 jioni kuwa kikao kimeisha na wajumbe wanaendelea kupiga kura kwa majina yale yale, akimaanisha aliyoyatangaza mapema asubuhi.
Waliopigiwa kura ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe, Waziri wa Ujenzi Dk John Magufuli na Waziri wa Katiba na Sheria Dk Asha-Rose Migiro.
Wengine ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba na Balozi wa Umoja wa Afrika (AU) katika Marekani, Amina Salum Ali.
Upigaji kura huo utachuja majina ya wagombea hao na kubaki matatu ambayo yalitarajiwa kupigiwa kura katika Mkutano Mkuu wa CCM, uliotarajiwa kuanza jana saa tatu usiku.
Aidha, Balozi Amina aliwasili ukumbini hapo baada ya upigaji kura kuanza akifuatana na mmoja wa watu wake wa karibu, aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa UWT, Halima Mamuya.
Balozi Amina na Dk Magufuli si wajumbe wa NEC, lakini kwa muda mrefu, Waziri huyo wa Ujenzi alikuwa katika jengo la White House na kabla ya kuanza kwa kikao cha NEC, alikuwa akiomba kura.
Pia ilielezwa kuwa Lowassa alikuwa abaki ndani baada ya kuitwa kuzungumza na Wazee baada ya kikao cha NEC, huku mitandao ya kijamii jana ikimhusisha na kukihama chama hicho tawala.
Baadae kikao cha NEC kilipitisha majina matatu ambayo yalifikishwa katika Mkutano Mkuu kumpata mgombea wa Urais kupitia tiketi ya CCM. Waliopitishwa ni Dk John Magufuli, Balozi Amina Salum Ali na Dk Asha-Rose Migiro.
Subscribe to:
Posts (Atom)